KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, August 12, 2012

TOT KUVAMIA TANGA IDDI EL FITRI


KIKUNDI cha taarab cha Tanzania One Theatre (TOT) kinatarajiwa kuvamia mkoani Tanga na kufanya maonyesho kadhaa wakati wa sikukuu ya Idd El Fitr.
Katibu wa TOT, Gasper Tumaini amesema leo kuwa, watayatumia maonyesho yao mjini Tanga kutambulisha albamu zao mbili mpya za Full Stop na Mjini Chuo Kikuu.
Tumaini amesema baada ya maonyesho yao ya Tanga, kundi hilo linaloongozwa na Malkia wa Mipasho nchini, Khadija Omar Kopa litafanya ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Ameitaja mikoa hiyo kuwa ni Mwanza, Shinyanga, Geita, Mara na baadaye kuhitimisha ziara yao katika mikoa ya Tabora na Singida.
Akielezea ratiba yao ya Tanga, Tumaini alisema siku ya Iddi Mosi, watafanya onyesho kwenye ukumbi wa Bandari, Iddi Pili watarindima kwenye Uwanja wa Mkwakwani na Iddi Tatu kwenye ukumbi wa White House uliopo Muheza.
Mbali na Khadija, waimbaji wengine wa TOT wanaotarajiwa kuhanikiza maraha katika maonyesho hayo ni Ally Stars, Abdul Misambano, Mwanamtama Amir, Mariam Khamis na Mwasiti Suleiman.

No comments:

Post a Comment