KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, August 15, 2012

Mwanne aja na Dume Mashauzi


MWIMBAJI  wa muziki wa taarab, Mwanne Othman Sekuru, ambaye anatamba katika  wimbo  wa Vifuu Tundu alioshirikishwa na AT, ambao  pia ulipenya katika  tuzo za muziki za Kilimanjaro 2012, anatarajia
kuipua kibao kingine baada ya sikukuu ya Idd El Fitr.
Akizungumza mjini Dar es Salaam leo, Mwanne alisema wimbo huo unakwenda kwa jina la  ‘Midume Mashauzi.
Mwanne amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kupata raha kwani katika wimbo huo, ameachia  madongo, ambayo kama mtu atakuwa na tabia hizo, yatakuwa ni sawa kwake.
"Wimbo huo umetungwa na Mohammed Omari Mkwinda ‘Meddy’, ambaye mara baada ya kuutunga akaniletea, nami nikaweka maneno ya kutia nakshi,"alisema.
Aliyataja baadhi ya maneno hayo kuwa ni 'Watashindana, lakini watashindwa wenyewe', 'Huna thamani kama mkia wa mbuzi', 'Hufuniki wala hufukuzi nzi’.
Mbali ya kuwa  mwimbaji katika kundi la Jahazi Modern Taarab, Mwanne pia ni mtangazaji wa kipindi cha ‘Tamtam za Mwambao’ kinachorushwa katika kituo cha redio ya East Africa ‘EATV’.

No comments:

Post a Comment