KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, June 18, 2017

MKE WA PILI WA MZEE YUSSUPH AFARIKI KWA UZAZI AMANA




Aliyekuwa mfalme wa muziki wa Taarab Alhaj Mzee Yusuf, amefiwa na mke wake wa pili, Chiku Khamis Tumbo.

Mzee Yusuf amenukuliwa katika moja ya vyombo vya habari leo akisema kuwa, mkewe alifariki jana kwenye Hospitali ya Amana, Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo wa zamani wa kundi la Jahazi, alisema alimpeleka mkewe Amana, jana saa 10 alasiri, kwa ajili ya kujifungua na kwa bahati mbaya opereshini (upasuaji) iliyofanywa jioni, haikwenda salama na ikampoteza mkewe na mtoto aliyezaliwa.

Mazishi ya Chiku yanatarajiwa kufanyika leo jioni kwenye makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam. Marehemu Chiku ameacha watoto wawili.

1 comment:

  1. I heard some nice soothing Swahili Taarab music https://bit.ly/2wwhGg6 . If you are planning to travel to one of the East African beaches, They have nice music called the taarab that is allitle bit like arabic but with some nice tune. https://bit.ly/2KR8NRw.Enjoy

    ReplyDelete