KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, January 15, 2013

KIKUNDI CHA TAIFA CHA TAARAB CHATIA FORA SHEREHE ZA MAPINDUZI ZANZIBAR

KIKUNDI cha Taifa cha Taarab cha Zanzibar juzi usiku kilitia fora kwa kutoa burdani ya aina yake ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za sherehe za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kutokana na nyimbo zake zilizoisisimua hadhira.

Onyesho hilo la taarab lilifanyika katika ukumbi wa Salama Bwawani, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mwanamwema Shein na viongozi wengine mbali mbali wa serikali na vyama vya siasa.

Katika onyesho hilo, kikundi hicho kilitumbuiza kwa nyimbo mbali mbali zilizoimbwa na waimbaji wake mahiri na wenye sauti za kumtoa nyoka pangoni huku wapiga ala wakionyesha uhodari wao katika kupiga ala za kiasili.

Kikundi hicho kilianza onyesho hilo kwa wimbo wa 'Rais tunakupenda' ulioimbwa kwa pamoja na Asha Ali kutoka Pemba na Sihaba Juma kutoka Unguja.

Wimbo huo ulikuwa ukimpongeza Dk. Shein kwa juhudi zake katika kusimamia utawala bora na mikakati yake ya kuendeleza kiliko cha kisasa na pia kuongeza bei ya karafuu.

Wimbo huo pia ulimpongeza Dk. Shein kwa kuendelea kusimamia vyema amani na utulivu uliopo nchini, ambao ndiyo muhimili mkubwa wa maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Nyimbo zingine za kikundi hicho zilizotia fora katika onyesho hilo ni ‘Siri ya Moyoni’, ulioimbwa na Fauzia Abdalla, Chaguo ulioimbwa na Saada Mohammed, Mpewa hapokonyeki ulioimbwa na Mtumwa Mbarouk na ’Sema’, ulioimbwa na Fatma Issa.

Mwimbaji mwingine aliyetia fora katika onyesho hilo alikuwa Makame Faki, maarufu kwa jina la Sauti ya Zege, ambaye upigaji wake wa kinanda ulitia fora na kuwafanya watu waliohudhuria waliwazike.

Mkurugenzi wa Kikundi hicho, Iddi Suwedi naye alitia fora baada ya kuimba wimbo wake wa Kinacho wasumbueni, uliotungwa na Mohammed Ahmed wakati Hilda Mohamed alitia fora aliposhuka na kibao chake cha Ninavyokupenda wakati Ali Masoud aliteka hadhira kwa wimbo wake wa Hakika nakupenda.

No comments:

Post a Comment