KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, August 14, 2012

T MOTO TAARAB KUIPUA VIBAO SITA VIPYA


KIKUNDI cha muziki wa taarab cha Tanzania Moto Modern Taarab 'T-Moto'  kinatarajia kuipua vibao vipya sita baada ya kukaa kimya kwa muda.
Meneja na Ofisa Mipango wa bendi hiyo, Kaisi Mussa Kaisi, alisema jana kuwa, kwa sasa wapi katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kurekodi nyimbo hizo.
Kaisi alisema nyimbo hizo, ambazo zimetungwa katika ubora wa juu, zinatarajia kuteka soko na kulipandisha hadhi kundi hilo ambalo lipo katika mikakati ya kuliteka soko la muziki huo.
Alisema mara baada ya kurekodi nyimbo hizo, zitasambazwa na kupigwa katika redio na kisha kufuatia uzinduzi wa albamu utakaofanyika baadae mwaka huu.
Alizitaja baadhi ya nyimbo hizo kuwa ni  ‘Domo la Udaku’ (Jokha Kassim), ‘Behind The Cine’, ‘Wewe sio Daktari wa mapenzi’  ‘Mwanamke Hashuo’,  ‘Jipangeni Upya’ na   ‘Ubaya'. 
Baadhi ya waambaji watakaoimba nyimbo hizo ni Johka Kassim, Nyawana Fundikira, Nassor Hussein, Shinuna Kassim, Mwanahawa Chipolopolo na Aisha Masanja.

No comments:

Post a Comment