KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, January 29, 2014

THABIT ABDUL AIPELEKA MODERN TARADANSI STUDIO


KUNDI jipya la muziki wa taarab la Modern Taradansi, linaloongozwa na Thabiti Abdul, limeingia studio kurekodi nyimbo zake mpya tatu.

Akizungumza na Burudani wiki hii, Thabiti alisema wamerekodi nyimbo hizo kwenye studio za Sound Crafters, zilizoko Temeke, Dar es Salaam.

Thabiti, ambaye ni mtunzi na mpiga kinanda hodari nchini alisema, wamerekodi nyimbo hizo kwa lengo la kukitambulisha rasmi kikundi hicho.

Hata hivyo, Thabiti hakuwa tayari kutaja majina ya nyimbo hizo kwa madai kuwa, watazitangaza rasmi mwishoni mwa wiki hii.

Kiongozi huyo wa Modern Taradansi, pia hakuwa tayari kutaja majina ya wasanii wanaounda kikundi hicho kwa madai kuwa, watajulikana siku ya utambulisho.

"Kwa sasa ni mapema kuwataja wasanii wanaounda kundi letu na pia nyimbo zetu mpya. Tutafanya hivyo siku ya utambulisho,"alisema.

No comments:

Post a Comment