KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, January 29, 2014

DAR MODERN TAARAB SASA INATISHA, YANYAKUA NYOTA WAPYA KADHAA

Mwamvita Shaibu
Zubeda Mlamali

BAADA ya kujiimarisha kwa kunyakua wasanii mbalimbali wapya wa taarab kutoka katika vikundi vingine, kikundi cha Dar Modern kimeingia studio kurekodi albamu yake ya pili.

Nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo, zilirekodiwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye studio za Sound Crafters zilizoko Temeke, Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na kikundi hicho wiki hii imeeleza kuwa, albamu hiyo mpya itakuwa na nyimbo saba zilizoimbwa na wasanii tofauti.

Kwa mujibu wa taarifa, lengo la kurekodi albamu hiyo ni kutambulisha ujio mpya wa kikundi hicho baada ya kutumia fedha nyingi kunyakua waimbaji nyota kutoka vikundi mbalimbali maarufu vya muziki huo.

"Lengo letu ni kuifanya Dar Modern Taarab itishe na iwe na kikosi kizuri baada ya kunyakua wasanii wazuri,"imeeleza taarifa hiyo iliyotiwa saini na mmoja wa viongozi wa kundi hilo, Adam Mlamali.

Miongoni mwa waimbaji wapya wanaounda kundi hilo ni pamoja na mkongwe, Mwanahawa Ally, Mwamvita Shaibu, Husna Mlamali, Zubeda Mlamali na Mossy Suleiman.

Vibao vipya vilivyorekodiwa na kikundi hicho ni Oh my honey (Hassan Vocha), Naenda kwa mume wangu (Husna Mlamali), Sikuamini macho yangu (Mwamvita Shaibu), Malipo duniani (Zubeda Mlamali), Siwanyimi uzuri (Mwanahawa Ally).

Mlamali hakutaka kutaja jina la wimbo ulioimbwa na Mossy kwa madai kuwa, wanataka iwe 'sapraisi' kwa mashabiki wao.

"Huu wimbo utakuwa sapraisi kwa mashabiki wakati tutakapozindua albamu yetu,"alisema Mlamali.
Kwa mujibu wa Mlamali, uzinduzi wa albamu hiyo umepangwa kufanyika Februari 14 mwaka huu, kwenye ukumbi wao mpya wa Dar Modern Hall ulioko Magomeni, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment