KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Thursday, January 9, 2014

JAHAZI YAFAFANUA SABABU ZA KUPELEKA UZINDUZI MOROGORO



KIKUNDI cha taarab cha Jahazi kimefafanua kuwa, kimetoa ufafanuzi
kuhusu uamuzi wake wa kuuchagua mkoa wa Morogoro kuwa mwenyeji
wa utambulisho wa nyimbo zake mpya.
Taarifa iliyotolewa na kikundi hicho wiki hii imeeleza kuwa, onyesho la
utambulisho wa nyimbo hizo, zitakazokuwemo kwenye albamu mpya,
litafanyika Januari 31 mwaka huu kwenye ukumbi wa Tanzanite Complex.
Mmoja wa viongozi wa Jahazi, Mohamed Mauji amesema wameamua
kuuchagua mji wa Morogoro kwa vile wanao mashabiki wengi huko.
Mauji, ambaye ni mpiga gita mahiri la solo, amesema mji wa Morogoro ni
ngome yao ya pili kwa ukubwa baada ya Dar es Salaam.
"Mara zote Jahazi imekuwa ikitambulisha nyimbo zake mpya Dar es
Salaam, na baadaye kuzitambulisha mikoani, lakini safari hii tumeamua
kuanzia Morogoro,"alisema.

No comments:

Post a Comment