KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, January 29, 2014

MWANAHAWA: SIWEZI KUACHA KUIMBA TAARAB


MWIMBAJI mkongwe wa nyimbo za muziki wa taarab nchini, Mwanahawa Ally, amesema hawezi kuacha muziki huo kwa sasa kwa sababu ndio unaomwezesha kuendesha maisha yake.

Mwanahawa alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, sauti yake ndiyo kipaji alichopewa na Mungu kinachomwingizia kipato chake cha kila siku.

Mwanamama huyo, aliyejiunga na kikundi cha Dar Modern Taarab hivi karibuni alisema, ataachana muziki baada kujiona hawezi kuimba kama ilivyo kawaida yake.

"Labda itokee nimepatwa na ugonjwa ambao utanifanya nishindwe kabisa kuimba, lakini kwa sasa sifikirii kabisa kuacha muziki wa taarab,"alisisitiza.

Mwanahawa ni miongoni mwa wasanii wa kundi la Five Stars Modern Taarab waliopata ajali mwaka juzi mkoani Morogoro na kunusurika kufa. Katika ajali hiyo, wasanii tisa walipoteza maisha.

Kwa sasa, Mwanahawa na kundi lake la Dar Modern Taarab, wanajiandaa kwa uzinduzi wa albamu yao mpya, utakaofanyika Februari 14 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment