KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, January 29, 2014

ALLY J AKABIDHIWA FIVE STARS


ALIYEKUWA mmiliki wa kikundi cha muziki wa taarab cha Five Stars, Shaks amesema, ameamua kumkabidhi kundi hilo msanii Ally J.

Shaks alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, Ally J hakuwa mmiliki wa kundi hilo, isipokuwa alikuwa miongoni mwa wasanii waanzilishi na alikabidhiwa jukumu la uongozi.

"Wakati nalinunua kundi hili, Ally J alikuwa miongoni mwa wasanii niliowakuta na alikuwa miongoni mwa waanzilishi, hakuwahi kuwa mmiliki,"alisema.

Shaks alitoa ufafanuzi huo baada ya Ally J kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni akisema kuwa, Five Stars haiwezi kufa.

Majigambo hayo ya Ally J yalikuja baada ya Shaks kutangaza kulivunja kundi hilo wiki mbili zilizopita.

"Kwa sasa Ally J ana uwezo na haki ya kusema chochote kuhusu Five Stars kwa sasa nilimpa umiliki wa kundi hilo bure bila kumuuzia,"alisema Shaks.

Hata hivyo, Shaks alisema Ally J hana haki ya kuwamiliki wasanii wa kundi hilo kwa vile alishavunja mikataba yao na kuwaruhusu kujiunga na vikundi vingine.

No comments:

Post a Comment