KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, September 11, 2012

VIDEO YA DUNIA DUARA IPO TAYARI


VIDEO ya kibao cha Dunia Duara ya kundi la muziki wa taarab la Kings Modern Taarab, inatarajiwa kuanza kuonekana hivi karibuni kwenye vituo mbali mbali vya televisheni nchini.
Akizungumza na Spoti Leo, Mkurugenzi wa kundi hilo, Majaliwa Hamisi alisema kazi ya kurekodi video hiyo inatarajiwa kukamilika wiki hii.
Kibao hicho kipo kwenye albamu ya My Heart ya kundi hilo na kimeimbwa na mwimbaji mkongwe, Mwanahawa Ally, ambaye kabla ya kurejea Kings Modern alikuwa akiimbia kundi la T-Moto.
Mwanahawa, ambaye amewahi kupachikwa majina ya Kinyago cha Mpapure na Chipolopolo, alikiri hivi karibuni kuwa, hakuwa na furaha alipokuwa kwenye kundi la T-Moto kama ilivyo awapo Kings Modern.
Kibao cha My Heart kimeimbwa na Young Hassan Ally wakati kibao cha Full Style kimeimbwa na Hanifa Mpita, aliyejiunga na kundi hilo hivi karibuni akitokea Mashauzi Classics.
Kwa mujibu wa Majaliwa, kibao cha Riziki mwanzo wa chuki kilichoimbwa na mshindi wa shindano la Bongo Star Search mwaka jana, Mariam ndicho pekee, ambacho hakijatengenezewa video.
"Karibu vibao vyote vilivyomo kwenye albamu yetu mpya vimeshatengenezewa video zake, isipokuwa Riziki mwanzo wa chuki,"alisema.
CHANZO CHA HABARI: SPOTI LEO

No comments:

Post a Comment