KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Saturday, September 1, 2012

MZEE YUSUPH AFUNGUA KAMPUNI YA KUSAMBAZA KAZI ZAKE


MSANII wa mziki wa Taarabu nchini Mzee Yussuf ameamua
kufungua kampuni yake ya usambazaji ijulikanayo kama MY
Collection kwa ajili ya kusambaza kazi zake.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Meneja Mauzo wa
Kampuni hiyo Mussa Msuba amesema wameamua kufungua duka
kwa ajili ya kuuza CD NA DVD za bendi ya Jahazi inayongozwa na
Mzee Yussuf.
Duka hilo lililopo makutano ya barabara ya likoma na
Muhonda, linajihusisha na uzaji wa DVD za taarabu kwa jumla na
rejareja kwa ajili ya kuwaweka karibu wapenzi wake ili waweze
kupata burudani kupitia nyimbo zao kwa kuwaburudisha wakiwa
majumbani.
Msuba amesema kuwa Mzee Yusufu yupo mbioni kutoa albamu
yake ya mduara itakayokuwa hivi karibuni ambayo ni yake binafsi.
Mbali na hilo, bendi hiyo itatoa video yake ya Live za albamu zake
zote za Two in One,Kazi ya Mungu, Nakula ka Naksh
Naksh,tupendane, Daktari wa Mapenzi, ambazo zitakuwa madukani kwa
ajili ya kuwapa wapenzi wao burudani wakiwa majumbani mwao.
Naye Mzee Yussuf aliongeza kwa kusema ameanzisha kampuni yake
binafsi baada ya kuona kwamba kazi zake nyingi zimekuwa
zikichakachuliwa kutokana na kuwepo kwa wizi wa kazi za sanaa.
Kampuni yake imekuwa ikisambaza kazi zake kwa ajili ya kuogopa
kuibiwa kutokana na wimbi la kazi za wasanii nchini.
Duka lililopo mtaa wa Muhonda na Likoma kwa ajili ya CD za
Jahazi pekee.
Mbali na duka hilo mzee Yusufu anamiliki duka lingine la Nguo
lililopo Magomeni Mapipa kwa ajili ya kujiongezea
kipato chake.
Bendi ya Jahazi mpaka sasa imekwisha toa albam nane ambazo
zipo madukani zinauzwa kwa ajili ya watu wotekupata burudani
wakiwa majumbani mwao.
Kwa sasa bendi hiyo ipo mbioni kuachia albamu yake ya tisa
ambayo aijapewa jina inatarajiwa kuzinduliwa mwezo Octoba kwa
ajili ya kutoa burudani kwa wapenzi wao na kuwataka mashabiki
wao kuja kuangalia na kusikiliza nyimbo mpya popote pale
wanapotoa burudani zao katika kumbi mbalimbali za jijini Dar es
salaam.

No comments:

Post a Comment