KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, September 11, 2012

VIDEO ZA ALBAMU TATU ZA DAR MODERN TAARAB ZAKAMILIKA


KIKUNDI cha Dar Modern Taarab kimekamilisha kazi ya kurekodi video za albamu zake tatu ilizozizindua hivi karibuni kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine iliyopo Magomeni, Dar es Salaam
Mkurugenzi wa kundi hilo, Mridu Ally alisema wiki hii kuwa, video hizo za albamu zote tatu zilikamilika wiki iliyopita.
Mridu alisema picha za video hizo zilipigwa katika maeneo mbali mbali ya Jiji la Dar es Salaam na Bagamoyo na lengo lilikuwa kuzipa vionjo tofauti.
Mkurugenzi huyo alitamba kuwa, video hizo ni moto wa kuotea mbali na kuongeza kuwa, anaamini zitakuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki wao.
"Video za albamu zote tatu tumezitengeneza kwa umakini mkubwa na utaalamu wa hali ya juu, kilichobakia ni kuanza tu kuzisambaza kwa mawakala wetu,"alisema.
Mridu alisema tayari baadhi ya video hizo zimeshaanza kuonyeshwa katika vituo mbalimbali vya televisheni nchini kabla ya kuanza kuwafikia mashabiki.
Albamu hizo tatu, ambazo zilizinduliwa kwa mpigo ni Ndugu wa mume, Toto la Kiafrika na Ninauvua ushoga.

No comments:

Post a Comment