KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, September 11, 2012

ALBAMU YA SHAKILA YA MAMA NA MWANA YAJA


ALBAMU binafsi ya mwimbaji mkongwe wa taarab nchini, Shakila Saidi ya Mama na Mwana, imechelewa kukamilika baada ya binti yake kupatwa na matatizo.
Shakila kwa kushirikiana na binti yake wa kwanza, Mwape Kibwana walitarajia kutoa albamu hiyo, ambayo tayari walishaanza kurekodi nyimbo zake, lakini wameshindwa kuikamilisha baada ya binti huyo kuugua.
Shakila alisema wiki hii kuwa, binti yake huyo alikumbwa na matatizo ya uja uzito na kusababisha washindwe kukamilisha kazi hiyo kwa muda waliopanga.
"Binti yangu, ambaye nimeshirikiana naye kurekodi albamu hiyo amepata matatizo wakati wa uja uzito, ikawa bahati mbaya tumeshindwa kukamilisha kazi hiyo," alisema Shakila.
Naye Mwape alisema wanatarajia kuendelea na kazi hiyo baada ya afya yake kutengemaa. Alisema anaamini kazi hiyo itakamilika baada ya muda si mrefu.
Kwa mujibu wa Mwape, wanatarajia kukamilisha kazi hiyo baada ya kurejea kutoka Dodoma, ambako wamealikwa kwenda kutioa burudani.
CHANZO CHA HABARI: SPOTI LEO

No comments:

Post a Comment