KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, September 2, 2012

JAHAZI WAJA NA ALBAMU MPYA

Mmoja wa waimbaji wa kikundi cha Jahazi, Mariam Mwinjuma

Fatma Kassim, mmoja wa waimbaji wenye mvuto wa kundi la Jahazi

KIKUNDI cha taarab cha Jahazi kinatarajia kupakua albamu mpya hivi karibuni itakayojulikana kwa jina la Wasiwasi wako ndio maradhi yako.
Akizungumza na blogu ya rusha roho wiki hii, kiongozi wa kundi hilo, Mzee Yusuph alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo sita.
Mzee alisema tayari baadhi ya nyimbo zimeshakamilisha wakati zingine bado zipo kwenye hatua ya mwisho.
Kwa mujibu wa Mzee, miongoni mwa nyimbo zitakazokuwemo kwenye albamu hiyo ni Mgodi wa Dhahabu, ambao umeshaanza kusikika kwenye vituo mbali mbali vya redio nchini.
Mzee alisema amepania kufanya mabadiliko makubwa kwenye muziki wa taarab ili kuwapa mashabiki ladha tofauti badala ya ile waliyoizoea.
"Sisi kama Jahazi tunapenda tufanye kile kitu mashabiki wanapenda, hivyo tunawaahidi mambo mapya kabisa katika albamu yetu hii mpya,"alisema.
Albamu hiyo itakuwa ya tisa tangu kundi la Jahazi lilipoanzishwa mwaka 2006. Albamu zingine zilizopita za kundi hilo ni Tupendane wabaya waulizane, Wagombanao ndio wapatanao, Mpenzi chokolate, Daktari wa mapenzi, Two in one, VIP na My Valentine.

No comments:

Post a Comment