KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, April 15, 2013

BREAKING NEWSSSS, HAJI MOHAMED WA EAST AFRICAN MELODY AFARIKI DUNIA

 Habari zilizotufikia hivi punde zimeeleza kuwa, msanii mkongwe na muziki wa taraab wa  kikundi cha East African Melody,  Haji Mohamed 'Kijukuu cha Siti Bint Saad, amefariki dunia.

Kwa mujibu wa habari hizo, Haji amefariki dunia leo saa nne asubuhi  wakati akipelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam baada ya kuzidiwa na presha.

Taarifa zimeeleza kuwa, marehemu Haji  alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya sukari na presha kwa muda mrefu.

Kifo cha Haji kimetokea miezi michache baada ya msanii mwingine wa kundi hilo, Lamania Shaaban kufariki dunia kwa ugonjwa wa kisukari.

Mwili wa marehemu Haji ulitarajiwa kusafirishwa leo mchana kwa boti ya Azam Marine kupelekwa Zanzibar kwa ajili ya mazishi.

Mkurugenzi wa East African Melody, Hashim Salum amesema leo kuwa, alipata nafasi ya kuzungumza na marehemu asubuhi na kumwambia kwamba
alikuwa anakwenda hospitali kuonana na daktari wake.

Marehemu Haji ameacha mke na watoto watatu.
Mungu ailaze roho yake mahali pema.

No comments:

Post a Comment