KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, December 17, 2012

THABITI ABDUL AJA NA HABIBI



HUWEZI kuamini, lakini ndivyo ilivyo. Baada ya kutamba katika utunzi na upapasaji kinanda kwenye nyimbo nyingi za taarab, hatimaye mwanamuziki Thabiti Abdul ameamua kujitosa kwenye uimbaji.
Mwanamuziki huyo, ambaye pia ni mahiri katika muziki wa dansi, ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Habibi.
Thabiti ameimba kibao hicho kwa kushirikiana na baadhi ya wasanii wa kundi la Mashauzi Classic, ambalo yeye ni miongoni mwa wakurugenzi wake.
Mpiga kinanda huyo amekiimba kibao hicho kwa umahiri mkubwa, akimlalamikia kimwana, ambaye amekuwa akimtesa kimapenzi.
Wakati Thabiti akijitosa kwenye uimbaji taarab, mwimbaji mkongwe wa fani hiyo, Ally Hemed Star ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Ni wewe.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ally Star kuibuka na kibao cha taarab baada ya kuwa kimya kwa takriban miaka miwili.

No comments:

Post a Comment