KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, March 9, 2014

UZINDUZI ALBAMU YA NYONGA MKALIA INI WAFANA


 
 

Moja ya sehemu ambayo unaweza kumtambua msanii mzuri ni pale ambapo anaweza kuimba na kucheza na mashabiki wake wanaokuja kila mara kumuangalia kwenye shoo na matamasha tofauti.

Hassan Ally alidhihirisha uzuri na umahiri wake ambao haupo tu kwenye kuimba na kutunga mashairi lakini pia kutawala jukwaa na kucheza na mashabiki wake.

Kwa wale ambao hawakufika kwenye shoo ya jana kwa sababu tofauti tofauti nakushauri ukisikia huyu jamaa anafanya shoo nyingine,nenda ukahudhurie.

Kila shoo nzuri hupambwa na muunganiko wa maelewano na sapoti baina ya wasanii,na jana Kings Modern Taarab walifanya vizuri sana kwenye kumuunga mkono mwenzao.

Walitoa burudani nzuri sana iliyowafanya mashabiki waliofika watulie huku wakisubiri Hassan Ally.Baadhi ya wasanii kutoka Kings ambao walitoa burudani ni pamoja na Amina Mnyalu,Aysher Vuvuzela,Mwanahawa Chipolopolo.

Ingawa shoo ilichelewa sana kuanza ilia baada Kings walipoanza kazi mambo yalikuwa poa,Baada ya nyimbo kadhaa za Kings ndipo Joha Kassim akapanda stejini nae akatoa shoo kali kama kawaida yake.

Ndio Hassan Ally aliingia ukumbini kwa kuwasuprise mashabiki wake kupitia geti ambalo mara kwa mara huwa linafungwa huku akisindikizwa na ngoma.

Moja ya vitu ambavyo wengi walivipenda na kumshangilia sana ni kuwashukuru watu ambao walifanikisha shoo hiyo,huku akionyesha furaha yake na upendo kwa wote waliohudhuria.

Hassana Ally alijipanga sana kiasi cha kujua afanye nini na wakati gani,sio tu katika uimbaji lakini kucheza na vijana walioandalia kufanya kazi hiyo.

Kuna muda alishuka chini ya steji na kuanza kucheza na mashabiki wake kitu kilichowafanya wengi kuancha kucheza na kumuangalia jinsi walivyokuwa wanacheza vizuri sana tena kwa umoja wao.

“Wengi hawajui kuwa mimi nina mtoto,sasa leo nataka mumuone mwanamke niliyezaa naye” Hayo yalikuwa maneno na Hassan Ally ambapo alimuita ‘Nyonga mkalia Ini’ wake,ndio zipotoka shangwe kutoka kwa mashabiki.

Kabla ya Khadija Kopa Hajapanda stejini,Hassan Ally aliimba nyimbo “Nyonga Mkalia Ini” na Mr. Pendwa Pendwa. Lady with Confidence ilikuwa ni nyimbo moja wapo ambayo Malkia aliimba.

Ingawa Bi.Mwanahawa Ally na Mc Dida hawakuwepo,lakini shoo ilikuwa nzuri na ilipangilia sana kiasi cha kufanya watu kutowaulizia hao ambao hawakuwepo. Mwanahawa Chipolopolo alichukua jukumu la U-Mc na kwa maoni yangu aliufanyia haki sana,pia watangazaji Yunis Kanumba wa City Radio na Mwanne wa Eatv walitoa sapoti pia.

IMETOLEWA BLOGU YA NAKSHI 255

No comments:

Post a Comment