KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, March 5, 2014

NYONGO MKALIA INI KUZINDULIWA KESHO TRAVERTINE


MWIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini, Hassan Ally kesho anatarajiwa kufanya uzinduzi wa albamu yake mpya itakayojulikana kwa jina la Nyongo mkalia ini.

Akizungumza na Burudani juzi, Hassan alisema onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine, Magomeni, Dar es Salaam.

Hassan alisema albamu hiyo itakuwa ya kwanza kwake kuifanya kwa kujitegemea nje ya kundi lake la Kings Modern Taarab.

Kwa mujibu wa Hassan, maandalizi yote muhimu kwa ajili ya onyesho hilo yamekamilika na amewataka mashabiki wake kujitokeza kwa wingi kwa lengo la kumuunga mkono.

Hassan alisema uzinduzi huo utasindikizwa na burudani kutoka kwa waimbaji mahiri wa muziki huo, Mwanahawa Ally, Jokha Kassim, Khadija Kopa na kundi la Kings Modern Taarab.

Mwimbaji huyo machachari alianza kutambulika rasmi katika muziki wa taarab alipokuwa kundi la New Zanzibar Stars. Uimbaji wake maridhawa na sauti yake murua vilimwezesha kupata mashabiki lukuki.

Baadaye alihamia kundi la Kings Modern Taarab kabla ya kutua T Moto Modern Taarab, lakini hakudumu navyo kwa muda mrefu. Alirejea Kings Modern Taarab mwaka jana na amedumu na kundi hilo hadi sasa, akiwa mmoja wa waimbaji wake mahiri.

No comments:

Post a Comment