KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, March 9, 2014

THABITI ABDUL AJITOSA KWENYE MOVI

 Wengi wa wasanii wa taarab wana kipaji zaidi ya kimoja,wapo ambao wanaimba na kutunga wenyewe nyimbo zao kitu ambacho tumekizoea.pia katika tasnia hii ya taarab wapo wasanii ambao wanapiga vyombo na pia wanaimba wapenzi wengi hawjui hili.

Ukimzungumzia Thabit Abdul “Jiko la Jela” yeye amekwenda zaidi ya hapo licha ya kwamba ni muimbaji na mpiga mpiga vyombo lakini pia ni muigizaji mzuri.

Thabi Abdul kwa sasa amefanya filamu yake mwenyewe akishirikiana na baadhi ya mastaa  wa “Bongo Movies”, inayokwenda kwa jina la “Brother and Sister”.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu na na Thabit ambaye pia ni mtengenezaji wa filamu hiyo amesema,kazi hiyo imeshakamilika na ipo katika hatua za mwisho kuingia sokoni ili wapenzi wapate kuiona filamu hiyo

No comments:

Post a Comment