KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, June 12, 2013

MASHAUZI AFUTIWA MASHITAKA


Na Sylvia Sebastian,DSJ 
MWIMBAJI nyota wa taarabu nchini, Isha Ramadhani, maarufu kwa jina la Isha Mashauzi, ameachiwa huru na Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, Dar es Salaam kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yake bila kuacha shaka.
Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Matrona Luanda baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wake na Mashauzi na mshitakiwa mwenzake, Halima Shaaban kutoa utetezi wao.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Matrona alisema kuwa mahakama hiyo inawaachia huru Mashauzi na Halima, ambao walikuwa wakikabiliwa na shitaka la wizi wa mkoba uliokuwa na fedha taslim sh. 758,200 mali ya muuza duka Sarah Peter.
Alisema kuwa upande wa Jamhuri umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi ya washitakiwa bila ya kuacha shaka yoyote.
Mashauzi na mwenzake, walikuwa wakidaiwa kutenda kosa hilo, Aprili 20, mwaka huu, mtaa wa Mafia na Jangwani, walipoingia dukani kwa ajili ya kununua nywele bandia.
Wakati wa usikilizwaji wa shauri hilo, Sarah ambaye ni muuza duka la Veronica Taki, alidai kuwa washitakiwa waliingia dukani siku hiyo ya tukio saa moja kasoro usiku, ambapo walifanikiwa kuchukua pochi iliyokuwa na fedha hizo ambazo ni za mauzo ya siku.

No comments:

Post a Comment