KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Friday, July 19, 2013

JUMA MGUNDA 'JINO MOJA WA JAHAZI' AFARIKI



ALIYEKUWA mpiga gita la besi wa kikundi cha taarab cha Jahazi, Juma Mgunda 'Jino Moja' amefariki dunia.

Mgunda alifariki dunia Jumatano iliyopita kwenye hospitali ya Temeke, Dar es Salaam.
Msanii huyo alikuwa amelazwa kwenye hospitali hiyo kwa muda mrefu kutokana na kuugua ugonjwa wa kifua kikuu.

Mgunda alijipatia umaarufu mkubwa katika fani ya taarab kutokana na kupiga gita hilo kwa umahiri mkubwa katika nyimbo za Daktari wa mapenzi.

Katika sehemu ya wimbo huo, kiongozi wa Jahazi, Mzee Yusuph anasikika akimtaja kwa majina ya 'Juma Mgunda Jini Moja.'

Marehemu Mgunda alizikwa jana katika makaburi ya Tandika, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment