KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, May 5, 2014

KUMBUKUMBU YA MAREHEMU MOHAMED SLEYUM ZAHOR



SLEYUM MOHAMED ZAHOR (1922-2003)
HATIMAYE leo umetimiza miaka 11 tangu ulipofariki dunia mwaka 2003
baada ya kuugua kwa muda mrefu na kuzikwa katika makaburi ya Kigilagila,
Kiwalani, Dar es Salaam.
Kifo chako kimetuachia pengo na upweke mkubwa. Tunazikosa simulizi zako, maono yako, ucheshi wako, busara zako na hekima zako.
Unakumbukwa
sana na mke, Bibi Fatuma Rashid na watoto wako, Rashid, Pili, Amisa,
Shani, Asha, Saumu, Nuru na Hilali pamoja na wajukuu zako wote.
Hakika
sisi zote ni waja wa Mwenyezi Mungu na kwake lazima tutarejea.
Tunaamini maandiko ya kwamba kila chenye roho, lazima kitaonja mauti.
Mungu ailaze roho yako mahali pema, peponi. Amin

No comments:

Post a Comment