KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Friday, September 27, 2013

THABITI ABDUL AMWACHA SOLEMBA ISHA MASHAUZI


MKURUGENZI msaidizi wa kikundi cha taarab cha Mashauzi Classic, Thabiti Abdul amejiengua katika nafasi hiyo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya kundi hilo zimeeleza kuwa, Thabiti ameshawasilisha barua ya kujitoa kwenye  kundi hilo kwa mkurugenzi wake, Isha Mashauzi.

Hata hivyo, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na Abdul au Isha kuhusu uamuzi wake huo.

Thabiti ni mmoja wa wasanii wanaounda kundi la Five Stars Modern Taarab, lakini amekuwa akishiriki mara kwa mara kwenye maonyesho ya Mashauzi Classic.

Hivi karibuni, Isha alikaririwa akisema kuwa, Thabiti bado yupo kwenye kundi hilo na amekuwa akishiriki kwenye maonyesho mbalimbali.

Habari kamili kuhusu uamuzi huu utazipata hivi karibuni kupitia kwenye blogu yako ya Rusha Roho.

No comments:

Post a Comment