KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Friday, September 27, 2013

MZEE YUSUPH KUSTAAFU MUZIKI 2015


MWIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yusuph amesema anatarajia kustaafu kazi hiyo katika kipindi cha miaka miwili ijayo.

Mzee, ambaye ni kiongozi wa kikundi cha Jahazi. amesema uamuzi wake huo umelenga kuwapa nafasi vijana kuonyesha vipaji vyao.

"Ni vigumu sana kuacha muziki wakati kikundi chako kipo juu, lakini kwa kuwa nimeshaamua, lazima nitekeleze hilo,"amesema Mzee alipozungumza na blogu ya

"Sina muda mrefu mbele, nitaweka kipaza sauti pembeni ili kuwapisha vijana waendeleze tasnia hii,"aliongeza.

Mtunzi na mwimbaji huyo mwenye sauti yenye mvuto, amesema uamuzi wake huo unaweza kuwaumiza mashabiki wake, lakini hana lingine la kufanya zaidi ya kuutekeleza.

"Kwangu mimi ni maamuzi magumu sana kwa vile nitakiacha kitu ninachokipenda na mashabiki wamenizoea, lakini itabidi wakubaliane na maamuzi haya,"alisema mwimbaji huyo, ambaye pia amepachikwa jina la Mfalme.

Kwa mujibu wa msanii huyo, baada ya kustaafu muziki, atalazimika kukivunja kikundi chake cha Jahazi na kumpatia kila msanii haki anayostahili kwa ajili ya kuendeleza maisha yake.

"Ningependa wasanii nitakaowaacha, watafute bendi zingine za kufanyakazi kwa kipindi hicho ili waendelee kuimba na kukuza zaidi vipaji vyao,"alisisitiza.

No comments:

Post a Comment