KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Friday, December 26, 2014

MBILI MPYA ZA WAKALI WAO MODERN TARADANCE USIPIME



KUNDI la muziki wa taarab la Wakali Wao Modern Taradance limedhihirisha kuwa ni moto wa kuotea mbali katika taarab ya kisasa baada ya kuibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Siioni thamani ya pendo.

Kibao hicho kilichotungwa na kuwekwa muziki na kiongozi wa kundi hilo, Thabiti Abdul, kimeimbwa na mwanadada Asia Mariam.

Kibao hicho na kile cha Mtu Mzima hovyo, vimerekodiwa katika studio za Marlon Linje, na vimekolezwa vikorombwezo vyenye mvuto wa aina yake.

Kibao cha Siioni Thamani ya Pendo kimepigwa katika miondoko ya taratibu, ni rhumba fulani lililokwenda shule huku ndani yake kukiwa kumechombezwa vitu fulani kutoka kwa baadhi ya nyimbo maarafu.

Kwa mfano, kipo kipande ambacho kimetoholewa kutoka kwenye wimbo wa Makumbele, uliotamba na bendi ya Orchestra Maquis Original ya hapa nchini zaidi ya miaka 15 iliyopita.

Aidha utakutana pia na vipande kutoka kwa wimbo unaendelea kulitingisha bara la Afrika “Kuchi Kuchi (Oh Baby)” ulioimbwa na J’odie wa Nigeria.

Vibao hivyo vimerekodiwa siku chache baada ya kundi hilo kuzindua albamu yao ya kwanza, inayojulikana kwa jina la Kalieni Viti siyo Umbea”.

No comments:

Post a Comment