KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Wednesday, September 24, 2014

ABDUL MISAMBANO AFUFUKA, AJA NA MPYA ISEMAYO 'SI MIE NI MOYO'




Msanii mkongwe katika muziki wa miondoko ya taarabu nchini,  Abdul Misambano, ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la 'Si mie ni moyo'.

Hii ni mara ya kwanza kwa Misambano kutoa kibao kipya baada ya kuwa kimya kwa miaka kadhaa.

Msanii huyo aliyewahi kung'ara katika kikundi cha Tanzania One Theatre (TOT Plus), alisema hivi karibuni kuwa, alifanikiwa kurekodi kibao hicho hivi karibuni baada ya kukifanyia mazoezi kwa wiki
kadhaa.

Misambano amesema katika kibao hicho, kinanda kimepigwa kwa umaridadi mkubwa na mkali wa kupapasa ala hiyo, Omary Kisira.

Kwa wanaomkumbuka Misambano, alijipatia umaarufu mkubwa kupitia kibao chake cha Asu kilichotamba miaka ya 1990.

No comments:

Post a Comment