KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, August 5, 2013

AMIN-T MOTO BADO IPO HAI

MKURUGENZI wa kikundi cha taarab cha T Moto, Amin Salmin amesema kundi hilo bado lipo hai na limezidi kujiimarisha.

Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Salmin alisema wamepanga kuliimarisha kundi lao kwa kuongeza wasanii wengine sita kutoka makundi mbalimbali.

Salmin alisema wasanii hao watatoka katika vikundi vya Jahazi na Kings Modern Taarab, lakini hakuwa tayari kutaja majina yao.

Kwa mujibu wa Salmin, wasanii wanne watatoka Jahazi na wengine wawili kutoka Kings Modern Taarab.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa kundi la G5 taarab, Hamisi Slim amesema kundi lake lipo katika maandalizi ya kuipua nyimbo mpya nne.

Mbali na kupika nyimbo nne, Slim alisema kundi lake linatarajia kuendelea kujiimarisha kwa kuongeza wasanii wawili wapya. Hakuwa tayari kutaja majina yao.

No comments:

Post a Comment