KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Thursday, January 5, 2017

LEYLA: SIPENDI KUZUNGUMZA MAMBO YANAYOMUHUSU KHADIJA YUSSUF

MWIMBAJI nyota wa taarab wa kundi la Jahazi, Leyla Rashid, amesema kamwe katika maisha yake hapendi kuzungumza mambo yanayomuhusu Khadija Yussuf.

Leila, mke wa kiongozi wa zamani wa kundi hilo, Mzee Yussuf, amesema anashangazwa na kauli mbalimbali zinazotolewa na Khadija kuhusu ndoa yake.

Mwanamama huyo amesema mumewe hajawahi kumkataza kuimba taarab ama kumtishia kumuacha kama inavyodaiwa na Khadija.

Akizungumzia wimbo mpya wa Khadija, ambao unazungumzia ndoa yake na Mzee, Leyla alisema ameusikia lakini hawezi kuuzungumzia.

"Sina mpango wa kumpa mtu kiki (kumpa ujiko) na wala sifikirii. Najali mambo yangu,"amesema Leyla.

"Ninayemjua katika maisha yangu ni Mzee, sina haja na Khadija,"aliongeza.

Leyla alisema maelewano kati yake na mumewe yanaendelea vizuri na ndoa yao imezidi kuimarika kuliko ilivyokuwa awali.

Aidha, alisema suala la talaka siyo la ajabu kwa watu wenye ndoa na kwamba linaweza kumkuta mtu yeyote.

No comments:

Post a Comment