KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, August 21, 2016

JK, MAKAMU WA RAIS SAMIA WAONGOZA MAZISHI YA MAREHEMU SHAKILA SAIDI

HII ni picha aliyopiga kwa mara ya mwisho marehemu Bi Shakila Saidi alipohudhuria mkutano mkuu maalumu wa CCM uliofanyika Julai 23, mwaka huu mjini Dodoma
Rais mstaafu Jakaya Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Bi Shakila Saidi, Mbagala Charambe, Dar es Salaam jana.
MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan akitia saini kitabu cha maombolezo baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Bi Shakila Saidi
MKE wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye akimkaribisha Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan nyumbani kwa marehemu Bi Shakila Saidi
Makamu wa Rais akiwafariji baadhi ya ndugu wa marehemu
WAZIRI Nape akiteta jambo na mmiliki wa blogu ya Michuzi, Ankal Muhidin Issa Michuzi. Katikati ni Mwenyekiti wa Chama Cha Muziki wa Dansi, Athumani Msumari
BAADHI ya waumini wa dini ya kiislamu wakijiandaa kuuswalia mwili wa marehemu Bi Shakila
MAKAMU wa Rais akishiriki kwenye dua ya kumuombea marehemu Shakila
JENEZA lenye mwili wa Bi Shakila likipelekwa makaburini. PICHA KWA HISANI YA BLOGU YA MICHUZI NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

No comments:

Post a Comment