KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Saturday, May 4, 2013

ISHA MASHAUZI ATINGA KIZIMBANI



MWIMBAJI mahiri wa nyimbo za taarab nchini, Isha Mashauzi na mwenzake, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na shitaka la wiz wa fedha taslimu sh. 758, 200.
Isha na Halima Shabani (26) walipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, mbele ya Hakimu Matrona Luanda.
Karani wa mahakama hiyo, Blanka Shayo alidai kuwa, washitakiwa walitenda kosa hilo Aprili 20 mwaka uu saa 12 jioni katika mtaa wa Mafia na Jangwani, wilayani Ilala.
Alidai kuwa, Isha na Halima waliiba pochi ya Veronica Taki, iliyokuwa na fedha taslimu sh. 758, 200 kutoka dukani kwa Sarah Peter, kMWIMBAJI mahiri wa nyimbo za taarab nchini, Isha Mashauzi na mwenzake, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na shitaka la wiz wa fedha taslimu sh. 758, 200.
Isha na Halima Shabani (26) walipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, mbele ya Hakimu Matrona Luanda.
Karani wa mahakama hiyo, Blanka Shayo alidai kuwa, washitakiwa walitenda kosa hilo Aprili 20 mwaka uu saa 12 jioni katika mtaa wa Mafia na Jangwani, wilayani Ilala.
Alidai kuwa, Isha na Halima waliiba pochi ya Veronica Taki, iliyokuwa na fedha taslimu sh. 758, 200 kutoka dukani kwa Sarah Peter, kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, washitakiwa walikana shitaka hilo na walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Washitakiwa hao baada ya muda, walitolewa rumande kwa ajili ya kupatiwa dhamana baada ya kutimiza masharti.
Kila mshitakiwa alitakiwa awe na mdhamini mmoja watakaotia saini bondi ya sh. milioni 1.5. Kesi hiyo itatajwa tena Mei 14 mwaka huu.itendo ambacho ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, washitakiwa walikana shitaka hilo na walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Washitakiwa hao baada ya muda, walitolewa rumande kwa ajili ya kupatiwa dhamana baada ya kutimiza masharti.
Kila mshitakiwa alitakiwa awe na mdhamini mmoja watakaotia saini bondi ya sh. milioni 1.5. Kesi hiyo itatajwa tena Mei 14 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment