KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, November 10, 2014

TAARAB YA MIAKA MINNE YA UONGOZI WA DK. SHEIN Z'BAR

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar
Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akiwa na Viongozi wengine katika  Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne ya ushindi wa CCM katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana.[Picha na Ikulu.]
 Viongozi mbali mbali  waliohudhuria katika Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne ya ushindi wa CCM katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana wakifuatilia kwa makini wakati
vikundi mbali mbali vikiburudisha .[Picha na Ikulu.] 
 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (kutoka kushoto) Mama Pili Balozi na Mama Asha Suleiman Iddi wake wa Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi wakiwa katika Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne ya ushindi wa CCM katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana wakifuatilia kwa makini wakati vikundi mbali mbali vikiburudisha .[Picha na Ikulu.]
 Mwimbaji wa kikundi cha Zanzibar One Rukia Moriss alipoburidisha kwa wimbo “Achekwe hana stara”wakati wakati wa Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne ya ushindi wa CCM na kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana [Picha na Ikulu.]
 Kikundi cha Taifa cha Muziki wa Taarab cha Culture musical Club kilipotumbuiza wakati wa Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne  ya ushindi wa CCM na kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana [Picha na Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai wakiteta jambo wakati wa Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne ya ushindi wa CCM katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana wakifuatilia kwa makini wakati vikundi mbali mbali vikiburudisha .[Picha na Ikulu.]

Waimbaji wa Kikundi cha Zanzibar Modern Taarab Khadija Khamis na Marium Juma wakiimba wimbo wa  Pika Dk.Shein BigUp wakati wa Tamasha maalum la taarab ya kusherehekea miaka minne (4) ya ushindi wa CCM na kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, katika  Ukumbi wa Salama Hall Bwawani jana [Picha na Ikulu.]