KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, March 9, 2014

UZINDUZI ALBAMU YA NYONGA MKALIA INI WAFANA


 
 

Moja ya sehemu ambayo unaweza kumtambua msanii mzuri ni pale ambapo anaweza kuimba na kucheza na mashabiki wake wanaokuja kila mara kumuangalia kwenye shoo na matamasha tofauti.

Hassan Ally alidhihirisha uzuri na umahiri wake ambao haupo tu kwenye kuimba na kutunga mashairi lakini pia kutawala jukwaa na kucheza na mashabiki wake.

Kwa wale ambao hawakufika kwenye shoo ya jana kwa sababu tofauti tofauti nakushauri ukisikia huyu jamaa anafanya shoo nyingine,nenda ukahudhurie.

Kila shoo nzuri hupambwa na muunganiko wa maelewano na sapoti baina ya wasanii,na jana Kings Modern Taarab walifanya vizuri sana kwenye kumuunga mkono mwenzao.

Walitoa burudani nzuri sana iliyowafanya mashabiki waliofika watulie huku wakisubiri Hassan Ally.Baadhi ya wasanii kutoka Kings ambao walitoa burudani ni pamoja na Amina Mnyalu,Aysher Vuvuzela,Mwanahawa Chipolopolo.

Ingawa shoo ilichelewa sana kuanza ilia baada Kings walipoanza kazi mambo yalikuwa poa,Baada ya nyimbo kadhaa za Kings ndipo Joha Kassim akapanda stejini nae akatoa shoo kali kama kawaida yake.

Ndio Hassan Ally aliingia ukumbini kwa kuwasuprise mashabiki wake kupitia geti ambalo mara kwa mara huwa linafungwa huku akisindikizwa na ngoma.

Moja ya vitu ambavyo wengi walivipenda na kumshangilia sana ni kuwashukuru watu ambao walifanikisha shoo hiyo,huku akionyesha furaha yake na upendo kwa wote waliohudhuria.

Hassana Ally alijipanga sana kiasi cha kujua afanye nini na wakati gani,sio tu katika uimbaji lakini kucheza na vijana walioandalia kufanya kazi hiyo.

Kuna muda alishuka chini ya steji na kuanza kucheza na mashabiki wake kitu kilichowafanya wengi kuancha kucheza na kumuangalia jinsi walivyokuwa wanacheza vizuri sana tena kwa umoja wao.

“Wengi hawajui kuwa mimi nina mtoto,sasa leo nataka mumuone mwanamke niliyezaa naye” Hayo yalikuwa maneno na Hassan Ally ambapo alimuita ‘Nyonga mkalia Ini’ wake,ndio zipotoka shangwe kutoka kwa mashabiki.

Kabla ya Khadija Kopa Hajapanda stejini,Hassan Ally aliimba nyimbo “Nyonga Mkalia Ini” na Mr. Pendwa Pendwa. Lady with Confidence ilikuwa ni nyimbo moja wapo ambayo Malkia aliimba.

Ingawa Bi.Mwanahawa Ally na Mc Dida hawakuwepo,lakini shoo ilikuwa nzuri na ilipangilia sana kiasi cha kufanya watu kutowaulizia hao ambao hawakuwepo. Mwanahawa Chipolopolo alichukua jukumu la U-Mc na kwa maoni yangu aliufanyia haki sana,pia watangazaji Yunis Kanumba wa City Radio na Mwanne wa Eatv walitoa sapoti pia.

IMETOLEWA BLOGU YA NAKSHI 255

THABITI ABDUL AJITOSA KWENYE MOVI

 Wengi wa wasanii wa taarab wana kipaji zaidi ya kimoja,wapo ambao wanaimba na kutunga wenyewe nyimbo zao kitu ambacho tumekizoea.pia katika tasnia hii ya taarab wapo wasanii ambao wanapiga vyombo na pia wanaimba wapenzi wengi hawjui hili.

Ukimzungumzia Thabit Abdul “Jiko la Jela” yeye amekwenda zaidi ya hapo licha ya kwamba ni muimbaji na mpiga mpiga vyombo lakini pia ni muigizaji mzuri.

Thabi Abdul kwa sasa amefanya filamu yake mwenyewe akishirikiana na baadhi ya mastaa  wa “Bongo Movies”, inayokwenda kwa jina la “Brother and Sister”.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu na na Thabit ambaye pia ni mtengenezaji wa filamu hiyo amesema,kazi hiyo imeshakamilika na ipo katika hatua za mwisho kuingia sokoni ili wapenzi wapate kuiona filamu hiyo

Wednesday, March 5, 2014

NYONGO MKALIA INI KUZINDULIWA KESHO TRAVERTINE


MWIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini, Hassan Ally kesho anatarajiwa kufanya uzinduzi wa albamu yake mpya itakayojulikana kwa jina la Nyongo mkalia ini.

Akizungumza na Burudani juzi, Hassan alisema onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine, Magomeni, Dar es Salaam.

Hassan alisema albamu hiyo itakuwa ya kwanza kwake kuifanya kwa kujitegemea nje ya kundi lake la Kings Modern Taarab.

Kwa mujibu wa Hassan, maandalizi yote muhimu kwa ajili ya onyesho hilo yamekamilika na amewataka mashabiki wake kujitokeza kwa wingi kwa lengo la kumuunga mkono.

Hassan alisema uzinduzi huo utasindikizwa na burudani kutoka kwa waimbaji mahiri wa muziki huo, Mwanahawa Ally, Jokha Kassim, Khadija Kopa na kundi la Kings Modern Taarab.

Mwimbaji huyo machachari alianza kutambulika rasmi katika muziki wa taarab alipokuwa kundi la New Zanzibar Stars. Uimbaji wake maridhawa na sauti yake murua vilimwezesha kupata mashabiki lukuki.

Baadaye alihamia kundi la Kings Modern Taarab kabla ya kutua T Moto Modern Taarab, lakini hakudumu navyo kwa muda mrefu. Alirejea Kings Modern Taarab mwaka jana na amedumu na kundi hilo hadi sasa, akiwa mmoja wa waimbaji wake mahiri.

MWANAHAWA AWASHUKUA MAPROMOTA UCHWARA


MWIMBAJI mkongwe wa muziki wa taarab nchini, Mwanahawa Ally ameilalamikia tabia ya baadhi ya mapromota kutumia jina na picha yake kibiashara bila idhini yake.

Mwanahawa alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, amekuwa akikerwa na tabia hiyo kwa sababu mapromota hao wamekuwa wakitumia jina na picha zake kibiashara bila kufikia makubaliano nao.

Alisema baadhi ya mapromota wamekuwa wakitengeneza matangazo ya barabarani yakiwa na picha zake na kumtaja kuwa ni miongoni mwa waimbaji watakaoshiriki kwenye maonyesho fulani wakati si kweli.

Amewataka mapromota hao kuacha tabia hiyo mara moja, vinginevyo atawachukulia hatua za kisheria ili liwe fundisho kwa wengine.

“Sitopenda kusikia au kuona jina au picha yangu inatumika kutangaza shoo bila idhini yangu au uongozi wa bendi yangu. Mimi ni msanii wa Dar Modern Taarab na nitakuwa napatikana katika kikundi hiki kila ijumaa katika hoteli ya Travertine,"alisema.

Mwanahawa ameamua kuwatolea uvivu mapromota hao kutokana na baadhi yao kutumia jina lake kuwahadaa mashabiki wa muziki wa taarab.

MASHAUZI ASEMA HANA UGOMVI NA THABITI ABDUL


 
KIONGOZI wa kikundi cha muziki wa taarab cha Mashauzi Classic, Isha Mashauzi amesema hana ugomvi wowote na mmiliki mwenzake wa zamani wa kikundi hicho, Thabiti Abdul.

Isha alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, Thabiti aliondoka Mashauzi Classic kwa hiyari yake na alitoa taarifa kwa viongozi wenzake.

“Sijui kwa nini mtu anapofanya mazuri hawaongei. Kuhusu kuwa na mgogoro na Thabit, mimi  sijui kwani nilishawahi kufanya naye kazi katika bendi yangu kwa muda mrefu, na yeye mwenyewe alituita sisi viongozi kwa pamoja na kusema anaondoka ndani ya bendi,"alisema

Kwa mujibu wa Isha, Thabiti aliwaeleza viongozi wenzake kwamba yuko tayari kushirikiana na Mashauzi Classic wakati wowote atakapohitajika kufanya hivyo, lakini kwa sasa hawamuhitaji.

"Kusema ule ukweli, kwa sasa hatuna shida naye, muda ukifika kama tutamuhitaji, tutafanya hivyo,"alisema mwanamama huyo.

“Lakini bado nashangaa kwa nini watu wanaeneza kutokuelewana baina yetu, labda mumfuate yeye mumuulize, lakini kwa upande wangu haja ya mja ni kunena, muungwana ni vitendo, kwa hiyo sioni sababu ya kuanza kujibizana," alisisitiza Isha.

Isha alisema pia kuwa, amekuwa akishangazwa na maneno yaliyozagaa mitaani na miongoni mwa wasanii wenzake kwamba, anaringa wakati hana sababu ya kufanya hivyo.

"Nimringie nani wakati mabosi zangu ni mashabiki na wapenzi wetu? Bila wao nisingekuwa hapa nilipo kwa sasa. Sisi ni mwendo wa kazi na bendi yangu, waache waongee wanavyojisikia, sisi tunachapa kazi,"aliongeza.

Mwimbaji huyo wa zamani wa kundi la Jahazi amewaomba mashabiki wa Mashauzi Classic wakae mkao wa kula, kusubiri ujio wa albamu yao mpya wanayotarajia kuitoa hivi karibuni.