KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Thursday, May 16, 2013

ISHA MASHAUZI ALIKATAA KUPEKULIWA-SHAHIDI


SHIHIDI wa kwanza katika kesi ya wizi wa fedha inayomkabili msanii wa muziki wa taarabu, Isha Mashauzi, amedai kuwa msanii huyo aliingia sehemu ya ndani ya duka hilo na kuchukua pochi yenye fedha.

Akitoa ushahidi huo mbele ya Hakimu Matrona Luanda, shahidi huyo, Veronika Taki, alidai Isha aliingia dukani ambapo haparuhusiwi bila ruhusa yake na kukaa katika kiti cha mmiliki wa duka karibu na boksi ambalo linasadikiwa kuwa na pochi iliyokuwa na fedha hizo.


Matrona alisema shahidi wa pili ambaye ni mlinzi wa duka hilo, Michael amedai kuwa msanii huyo alikataa kupekuliwa.

Alidai kuwa, msanii huyo alikataa kupekuliwa baada ya kumfuatilia nyendo zake tangu alipotoka katika duka hilo na kuingia katika duka la jirani kutafuta nywele za bandia' wiving'.

Michael alidai hayo jana katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, mbele ya Hakimu Matrona Luanda, ambapo shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Katika kesi hiyo, Isha (28) na Halima Shabani (26), wanadaiwa Aprili 20, mwaka huu, saa 12.45 jioni, mtaa wa Mafia na Jangwani, maeneo ya Kariakoo bila halali na kwa makusudi waliiba pochi ya mkononi iliyokuwa na sh. 758,000 kutoka dukani kwa Sara Peter, mali ya Veronica Taki.

Akitoa ushahidi wake, Michael alidai siku ya tukio akiwa nje ya duka kwa ajili ya kulinda mali za nje, waliingia hao wateja na walikaa ndani kwa takriban saa moja wakichambua 'mawigi'.

Michael alidai akiwa nje, hakujua kilichokuwa kikiendelea ndani na kwamba baada ya wateja hao kutoka alimuona muuza duka akitoka na kumuambia pochi yake imeibiwa.

Alidai muuza duka huyo alimueleza walioiba pochi hiyo ni wateja waliotoka mwisho (Isha na Halima), na hivyo aliamua kuwafuatilia na kuwakuta katika duka la pili.

Shahidi huyo, alidai alipowafuatilia dukani kwa mara ya kwanza aliwaeleza waende kuchukua wivingi walilokuwa wakilitafuta kwani duka linataka kufungwa.

Alidai aaliwafuata tena kwa mara ya pili ambapo walimjibu kwamba wafunge duka na watoke na hilo wigi nje. Hata hivyo, alidai Isha na wenzake hawakurudi katika hilo duka na kwenda katika gari lao na alipowaeleza juu ya upotevu wa pochi walishangaa na kudai wao si wezi.

Shahidi huyo alidai mama mwenye nyumba alipowafuata, Isha alikataa kupekuliwa na kuacha namba zake za simu kwa madai anawahi kipindi. Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Mei 22, mwaka huu.
 

Saturday, May 4, 2013

ISHA MASHAUZI ATINGA KIZIMBANI



MWIMBAJI mahiri wa nyimbo za taarab nchini, Isha Mashauzi na mwenzake, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na shitaka la wiz wa fedha taslimu sh. 758, 200.
Isha na Halima Shabani (26) walipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, mbele ya Hakimu Matrona Luanda.
Karani wa mahakama hiyo, Blanka Shayo alidai kuwa, washitakiwa walitenda kosa hilo Aprili 20 mwaka uu saa 12 jioni katika mtaa wa Mafia na Jangwani, wilayani Ilala.
Alidai kuwa, Isha na Halima waliiba pochi ya Veronica Taki, iliyokuwa na fedha taslimu sh. 758, 200 kutoka dukani kwa Sarah Peter, kMWIMBAJI mahiri wa nyimbo za taarab nchini, Isha Mashauzi na mwenzake, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na shitaka la wiz wa fedha taslimu sh. 758, 200.
Isha na Halima Shabani (26) walipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, mbele ya Hakimu Matrona Luanda.
Karani wa mahakama hiyo, Blanka Shayo alidai kuwa, washitakiwa walitenda kosa hilo Aprili 20 mwaka uu saa 12 jioni katika mtaa wa Mafia na Jangwani, wilayani Ilala.
Alidai kuwa, Isha na Halima waliiba pochi ya Veronica Taki, iliyokuwa na fedha taslimu sh. 758, 200 kutoka dukani kwa Sarah Peter, kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, washitakiwa walikana shitaka hilo na walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Washitakiwa hao baada ya muda, walitolewa rumande kwa ajili ya kupatiwa dhamana baada ya kutimiza masharti.
Kila mshitakiwa alitakiwa awe na mdhamini mmoja watakaotia saini bondi ya sh. milioni 1.5. Kesi hiyo itatajwa tena Mei 14 mwaka huu.itendo ambacho ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, washitakiwa walikana shitaka hilo na walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Washitakiwa hao baada ya muda, walitolewa rumande kwa ajili ya kupatiwa dhamana baada ya kutimiza masharti.
Kila mshitakiwa alitakiwa awe na mdhamini mmoja watakaotia saini bondi ya sh. milioni 1.5. Kesi hiyo itatajwa tena Mei 14 mwaka huu.